The House of Favourite Newspapers

Yanga Kuwashusha Majembe Manne Dirisha Dogo

0

KUELEKEA kwenye usajili wa dirisha dogo litakalofunguliwa Desemba 15, mwaka huu na kufungwa Januari 15, mwakani, Yanga imejipanga kuboresha eneo lake la ulinzi upande wa kulia na kushoto.

 

Katika kuimarisha huko, tayari ipo kwenye mazungumzo na mabeki wawili waliowahi kuitumikia timu hiyo, Hassan Kessy na David Luhende.

 

Yanga katika eneo la beki wa kulia, wanacheza Kibwana Shomary na Paul Godfrey ‘Boxer’, huku upande wa kushoto akiwa Yassin Mustafa na Adeyum Saleh.

Chanzo kutoka ndani ya Yanga kimeliambia Spoti Xtra kwamba, tayari Yanga imeshaingia kwenye mazungumzo na Luhende anayecheza Kagera Sugar na Kessy anayekipiga Mtibwa Sugar na kama mambo yataenda sawa basi watasajiliwa.

 

“Timu yetu bado ipo kwenye maboresho madogo, hivyo utaona kocha wetu Cedric Kaze anaendelea kuangalia nafasi muhimu za kuongeza ili tuunde kikosi chenye ushindani sahihi, hivyo tunatarajia kuongeza mabeki wawili, kulia na kushoto.

 

“Katika nafasi hizo tunategemea zaidi kuongeza wazawa hasa David Luhende na Hassan Kessy ambao tuna mazungumzo nao, kama tutaafi kiana tutawasajili.“Ikishindikana, basi kocha amesema ataangalia uwezekano wa kuangalia mchezaji kutoka nje ya Tanzania wa nafasi hizo ili amsajili,” kilisema chanzo.

 

Wakati taarifa zikiwa hivyo, Ofi sa Mhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz, aliliambia Spoti Xtra kuwa: “Tuna kama wiki moja kuelekea dirisha la usajili kufunguliwa, Wanayanga watulie, tutafanya usajili makini kuimarisha sehemu ambazo zina mapungufu.”Wengine wanaotajwa kujiunga na Yanga katika usajili wa dirisha dogo ni Eric Rutanga na Meshack Abraham.

Leave A Reply