The House of Favourite Newspapers

Yanga: Tuleteeni Yeyote Kombe la Shirikisho la Azam

0

BAADA ya kuifungashia virago Tanzania Prisons na kutinga robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam marufu Kombe la FA, uongozi wa Klabu ya Yanga umetema cheche kuwa hawaihofii timu yoyote watakayocheza nao, hivyo wako tayari.

 

Yanga wametinga hatua hiyo baada ya juzi Ijumaa kuwafunga Prisons bao 1-0 katika mchezo mkali wa hatua ya 16 bora uliopigwa kwenye Uwanja wa Nelson Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Haji Mfikirwa, alisema: “Kwanza kabisa tunashukuru kwa kufikia hatua hii ya robo fainali, huu ni mwendelezo wa malengo ambayo tumejiwekea msimu huu.

“Tayari tumechukua Kombe la Mapinduzi, na sasa tunapambana kuhakikisha tunatinga fainali na kutwaa kombe hili la FA.

 

“Tunajua wazi haitakuwa kazi rahisi kutokana na ugumu wa michuano hii, kwani kila mmoja ameona mchezo wetu ulivyokuwa mgumu, lakini niwahakikishie kuwa tumejipanga vizuri na hatuihofii timu yoyote tutakayopangwa nayo. Tumejipanga kucheza kila mchezo kama fainali ili kutimiza lengo letu.

 

“Katika kuongeza motisha juu ya hilo, uongozi umejipanga vizuri kuongeza hamasa ndani ya kikosi chetu katika namna mbalimbali ikiwemo bonasi za wachezaji kuelekea hatua zinazofuata.

Leave A Reply