The House of Favourite Newspapers

Yanga Waomba Mwamuzi Abadilishwe

0

Uongozi wa Klabu ya Yanga Sports Club, umesema umeshtushwa na na chaguo la Mwamuzi Ahmed Arajiga kuchezesha mchezo wa Fainali za Kombe la Shirikisho (ASFC) utakaochezwa Kigoma Jumapili hii Julai 25.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na idara ya habari ya klabu hiyo, hali hiyo imetokana na kuwa mwamuzi huyo amechezesha mechi zilizofuatana za wapinzani wao Simba katika mashindano hayo katika hatua ya Robo Fainali, Nusu na sasa Fainali.

Taarifa hiyo imeeleza, kitendo cha kumrudia mwamuzi huyo katika mechi tatu za timu moja na shindano moja, kimewatia mashaka hivyo wanaomba TFF watafakari juu uamuzi wa kumtumia mwamuzi huyo.

Written by @erick.evarist cc @hotpot_tz

Leave A Reply