The House of Favourite Newspapers

Yanga Yaichapa African Lyon 1-0

Kikosi cha Yanga kimeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya African Lyon katika mchezo wa kirafiki uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Bao pekee la Yanga limewekwa kimiani na Yusuph Mhilu mnamo dakika za mwisho za mchezo.

Yanga wametumia mechi hiyo kama maandalizi ya kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu Bara.

Katika kipute hicho, Yanga imewakosa nyota wake baadhi ikiwemo Kelvin Yondani, Thaban Kamusoko, Juma Mahadhi walio majeruhi na wengine waliokuwa Uganda kwa majukumu ya timu ya taifa.

Comments are closed.