Yanga Yaipiga JKT Tanzania 3-0, Makambo na Ngassa Kama Kawa
TIMU ya Yanga imeshinda bao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania leo katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu Bara. Wafungaji wa Yanga ni Heritier Makambo dakika ya 27 kipindi cha kwanza, Mrisho Ngassa dakika ya 54 na Ibrahim Ajibu dakika ya 81 kipindi cha pili.
Ushindi wa Yanga unamfanya afikishe pointi 35 na kupanda mpaka nafasi ya kwanza nyuma ya Azam FC wenye pointi 33 na Simba akiwa katika nafasi ya tatu akiwa na pointi 27 akicheza michezo 12.
PICHA: RICHARD BUKOS | GPL
Comments are closed.