Yanga Yawasili Kuwavaa TP Mazembe
Baadhi ya wachezaji wa Yamga wakipita kwenye mashine za ukaguzi.
Kikosi cha Yanga ambacho kilianza kurejea hapa nchini kwa mafungu kuanzia jana alfajiri kikitokea Uturuki kilikoweka kambi kabla ya kuivaa TP Mazembe ya Kongo DRC, leo alfajiri wachezaji wengine wa kikosi hicho waliwasili kwa ajili ya mchezo huo unaotarajiwa kupigwa keshokutwa Jumanne katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Wachezaji hao waliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere saa nane na
nusu usiku.
Hivi ndivyo mambo yalivyokuwa.
Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima, akimweleza jambo meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh.
Kifaa kipya cha Yanga kilichotokea Coastal Union ya Tanga, Juma Mahadhi.
Beki mpya wa Yanga aliyetokea Simba, Hassan Kessy, naye alikuwepo kwenye safari hiyo.
Beki, Vincent Bossou.
Mbuyu Twite, hivi ndivyo alivyopokelewa na wadada hawa ambao walikuwa wakiongea Kikongo.
Deus Kaseke.
Kipa wa Yanga, Deogratius Munishi ‘Dida’.
PICHA : RICHARD BUKOS / GPL