The House of Favourite Newspapers

Yondani, Tambwe wazua hofu Yanga

0

AmissTambwe2

Mshambuliaji wa Yanga Hamis Tambwe.

Sweetbert Lukonge, Dar es Salaam
HOFU kubwa imetanda ndani ya kikosi cha Yanga kutokana na hivi karibuni kukumbwa na wimbi la majeruhi wakati ikikabiliwa na mchezo mgumu ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mwadui FC utakaofanyika Jumatano hii kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Miongoni mwa wachezaji ambao wamekumbwa na majeraha ni Amissi Tambwe na Kelvin Yondani.

Hata hivyo, Tambwe na Yondani licha ya kuwa majeruhi, wameondoka na kikosi cha timu jijini Dar na kwenda Shinyanga tayari kwa kuivaa Mwadui FC, lakini haijulikani kama watakuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Inadaiwa majeraha hayo waliyapata katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Toto Africans ya Mwanza uliofanyika Jumatano iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kuwafanya washindwe kufanya mazoezi ya nguvu na wenzao hivi karibuni kabla ya jana kwenda mkoani Shinyanga.

Hali hiyo inamnyima usingizi kocha mkuu wa timu hiyo, Mholanzi, Hans van Der Pluijm ambaye jana kabla ya safari hiyo ya kwenda Shinyanga, aliliambia gazeti hili kuwa hajui kama anaweza kuwatumia katika mechi hiyo na anachosubiri ni taarifa ya daktari wa klabu hiyo, Shecky Mngazija.

Alipoulizwa Mngazija kuhusiana na hali ya wachezaji hao, alisema kuwa wanaendelea vizuri kwani mamuvu yaliyokuwa yakiwakabili yalikuwa ni ya kawaida na Mungu akipenda kufikia Jumatano watakuwa fiti na tayari kwa kupambana na Mwadui FC.

“Hivi sasa wanaendelea vizuri na tayari wameshaanza kufanya mazoezi mepesi baada ya kuwapatia tiba, hivyo ni matumaini yangu kuwa mpaka kufikia Jumatano watakuwa fiti kwa asilimia mia moja.

“Yondani alikuwa anahisi maumivu ya nyonga na Tambwe alikuwa anasumbuliwa na maumivu ya msuli wa mgongoni, baada ya kupatwa na hali hiyo niliwapumzisha kwa muda ili niweze kuwapatia tiba na sasa wapo vizuri, hivyo kocha asiwe na shaka yoyote, uamuzi wa kuwatumia au kutowatumia utakuwa ni wake,” alisema Mngazija.

Leave A Reply