The House of Favourite Newspapers

Zahera: Simba Itaifunga AS Vita Nje Ndani

0

LIYEKUWA Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera raia wa DR Congo, amefi chua kuwa Simba wana nafasi kubwa ya kushinda mechi zote mbili dhidi ya AS Vita.Zahera ameongeza kwamba, hiyo ni kutokana na AS Vita kukosa wachezaji wenye uzoefu wa kutosha.

“Naona nafasi kubwa ya kufanya vizuri ipo kwa upande wa Simba kwa sababu vitu vinabadilika kadiri muda unavyokwenda, haiwezi kuwa kama ilivyokuwa wakati ule kutokana mabadiliko makubwa yaliyofanywa na AS Vita.“

 

Sioni dalili za wao kuwafunga Simba msimu huu katika hatua hiyo kwa kuwa Simba bado ina wachezaji wenye uzoefu na wapo pamoja kwa muda mrefu tofauti na AS Vita ambayo ina wachezaji wengi wapya na hawana uzoefu wa michuano ya hiyo,” alisema Zahera.

Leave A Reply