WATU wasiopungua 384 wamefariki dunia baada ya tetemeko la ardhi na kimbunga cha tsunami kuikumba Indonesia.
Habari kutoka jiji la Palu katika kisiwa cha Sulawesi zinasema mamia ya watu wamejeruhiwa na maelfu ya nyumba zimeharibiwa kutokana na dhoruba iliyosababishwa na mawimbi yaliyokuwa na urefu wa zaidi ya mita mbili.
Wengi wa waliofariki walikuwa katika ufukwe wa Palu, mji mkuu wa jimbo la Sulawesi Kati, ambapo ulifunikwa na taka na vifusi mbalimbali.
“Tsunami hiyo ilitokea jana, wakati watu walikuwa wakiendelea na shughuli zao ufukweni, na kwa vile ilikuja ghafla, hawakuweza kukimbia,” alisema ofisa mmoja anayeshughulikia majanga, Sutopo Purwo Nugroho.
Comments are closed.