Zaidi ya Wanafunzi 70 Wanusurika Kifo Baada ya Bweni Lao Kuteketea kwa Moto
ZAIDI ya wanafunzi 70 katika shule ya wavulana ya Bwiru Sekondari iliyopo manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza wamenusurika kifo baada ya bweni kuteketea kwa moto.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 3:40 usiku wa kuamkia leo wakati wakiwa madarasani wakijisomea masomo yao ya ziada.
Tayari Mamlaka husika zinaendelea na uchunguzi ili kujua chanzo cha tatizo ingawa madhara ni makubwa ikiwemo kuteketea kwa mali za wanafunzi pamoja na kuharibika kwa miundombinu ya shule.