The House of Favourite Newspapers

Zari Apiga Kambi Kumdhibiti Mobeto

Zarina Hassan ‘Zari’ .

 

Wakati kukiwa na figisufigisu kuhusu uhusiano kati ya wadada wawili waliozaa na mwanaume mmoja, Zarina Hassan ‘Zari’ na Hamisa Mobeto, mwanamke huyo mama wa watoto watano anayeishi Afrika Kusini, anadaiwa kutua jijini na kuweka kambi maalum kulinda kitumbua chake, Risasi Mchanganyiko limeambiwa.

 

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho karibu na Zari, inadaiwa kuwa mjasiriamali huyo alikuwa jijini Dar es Salaam ambako alihudhuria shughuli mbili za watu wake wa karibu, lakini inadaiwa kuwa hiyo ilikuwa ni geresha tu, kwani ziara yake ya kushtukiza ilikuwa na lengo maalum.

“Unajua kuna mambo kidogo kama hayaeleweki ambayo Mobeto anafanya, sasa Zari amepiga hesabu na kuamua kujiongeza, amekuja mjini na kupiga kambi Madale kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, katika matukio yote mawili alihudhuria na mzazi mwenzake, kitu ambacho kilimnyima kabisa nafasi Mobeto ya kusogelea,” alisema mtoa habari wetu.

Hamisa Mobeto.

Kumekuwa na uvumi kuwa Mobeto ameongea na kumalizana na mzazi mwenzake nje ya vyombo vya kisheria na baadhi wakidai kuwa wamerejesha hata uhusiano wao, kitu ambacho kinamfanya Zari kuishi kimachalemachale.

 

Katika video vilizowekwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ilimuonyesha Zari akiwa na furaha tele, tofauti na mzazi mwenziye aliyeonekana kama kuna jambo ambalo hafurahishwi nalo. Zari raia wa Uganda, anaishi Afrika Kusini pamoja na watoto wake watano, wakiwemo watatu aliozaa na mumewe, Ivan Ssemwanga aliyefariki mapema mwaka huu.

 STORI: MWANDISHI WETU, Risasi MCHANGANYIKO | DAR ES SALAAM

Comments are closed.