The House of Favourite Newspapers

Binti miaka 8 afanyiwa ukatili wa kutisha!

0

mtoto ateswa picha na global publishers (1)

Mtoto Mariam aliyezibwa uso.

Na Issa Mnally, UWAZI

DAR ES SALAAM: Mtoto aliyejulikana kwa jina moja la Mariam (10), mkazi wa Mavurunza ‘A’ Kimara King’ong’o, Dar yupo katika mateso makubwa kufuatia vitendo vya ukatili na unyanyasaji anavyofanyiwa na mwanamke anayedaiwa kuwa ni mama yake mzazi aitwaye Aisha.

mtoto ateswa picha na global publishers (5)Akionesha sehemu ya shingo alivyokwaruzwa kwa kucha.

Kwa mujibu wa majirani, mtoto huyo ambaye hata mahudhurio yake shuleni si mazuri, amekuwa katika mateso hayo ya kupigwa mpaka kujeruhiwa kwa muda mrefu lakini majirani walikuwa wakishindwa jinsi ya kumnasua kuzingatia kuwa, anayedaiwa kufanya vitendo hivyo ni mama yake.

mtoto ateswa picha na global publishers (2)Hivi karibuni, majirani wa eneo hilo wakishirikiana na Mjumbe wa Shina Namba 063, Mavurunza ‘A’ Kwa Kichwa, Janet Moshi waliamua kumwokoa mtoto huyo baada ya kufukuzwa nyumbani na mama yake huyo majira ya saa 4:30 usiku bila kuwa na sehemu ya kwenda.

mtoto ateswa picha na global publishers (3)“Ilikuwa saa nne na nusu usiku, sisi tulikuwa tumekaa kule mbele tukipata moja moto, moja baridi (pombe) ndipo tukasikia kelele za mama wa mtoto akimfokea bintiye huku akimpiga na  kumfukuza  atoke nyumbani kwake,” alisema mama Mayunga mmoja wa akina mama walioamua kujitoa kumsaidia mtoto huyo.

“Kila siku anampiga huyu mtoto. Unayaona hayo majeraha? Yote yametokana na kipigo ambacho  anakipata kutoka kwa mama yake,” alisema mama Donata huku akimgeuzageuza mtoto huyo sehemu ya shingo ili kuonesha majeraha hayo.

mtoto ateswa picha na global publishers (4)Kwa mujibu wa mtoto mwenyewe, ambaye anaweza kujieleza kwa ufasaha, anawashukuru mama Mayunga, mjumbe wa shina na mama Donata kwa kumtoa mdomoni mwa ‘mamba’ kwani alikuwa katika mateso makubwa.

“Nilikuwa nafanyiwa unyama wa kutisha na mama, ananipiga, ananifinya, ananigongesha ukutani mpaka natokwa na damu nyingi hadi zinakauka zenyewe.

“Siku nyingine aliniambia ataniua halafu aniweke kwenye kiroba na kwenda kunitupa porini. Chakula sili nikashiba, mengine hayaelezeki,” alisema mtoto huyo.

Juzi, Uwazi lilimtafuta mama wa mtoto huyo kwa njia ya simu lakini ikapokelewa na mwanaume aliyesema ni mume au baba wa mtoto huyo ambaye alisema:

“Mimi siwezi kusema lolote kuhusu ishu hiyo kwa sababu suala lenyewe lipo polisi.”

Uwazi: “Basi uje ofisini kwetu tuliongelee hili suala la mtoto wako.”

Baba: “Mimi huko ofisini kwenu siwezi kuja.” (akakata simu).

Hata hivyo, kwa mujibu wa mjumbe wa nyumba kumi, suala hilo limepelekwa Kituo cha Polisi Kimara na kuandikishwa kwa faili lenye kumbukumbu KIM/2858/016 TAARIFA. Pia, akina mama hao walimpeleka mtoto huyo kwenye Zahanati ya Serikali, Kimara na kupewa fomu ya polisi namba tatu (PF3) yenye namba KMR/10791/2016 SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI.

Leave A Reply