The House of Favourite Newspapers

Tazama picha za mazishi ya Ndanda Kosovo katika makaburi ya Kinondoni

0

085A9851

IMG_6672

IMG_6702

IMG_6704

IMG_6697

IMG_6626

IMG_6633

IMG_6681DSC_0887

IMG_6275

IMG_6300

IMG_6346

IMG_6352

IMG_6363

IMG_6381
IMG_6443

IMG_6491

IMG_6544

IMG_6589

WAZIRI wa Habari, Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda wamewaongoza mamia ya waombolezaji katika shughuli ya mazishi ya staa wa Muziki aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita, Ndanda Kosovo ‘Kichaa’ katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar,

Mwanamuziki huyo Ndanda Kosovo ‘Kichaa’ amezikwa leo Jumatano kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar ambapo maandalizi yamefanyika kwenye nyumba ya Ubalozi wa Congo DRC iliyopo Kinondoni-Hananasif jijini.

Dodoo alisema wameamua kumzika marehemu hapa nchini kufuatia wosia wake alioutoa mbele ya Waziri wa Habari, Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye wakati akizungumza na wanamuziki wa dansi katika Ukumbi wa Vijana Kinondoni mwezi uliopita.

Katika kikao hicho Ndanda alisimama na kusema endapo akifa basi maiti yake izikwe hapa Tanzania kwa kuwa ndipo mahali alipopatia mafanikio makubwa ya kimuziki na anahisi ndiyo sehemu ambayo atazikwa na watu wengi kuliko Lubumbashi alikozaliwa.

DENIS MTIMA NA RICHARD BUKOS/GPL

Leave A Reply