MSTAHIKI Meya wa Jimbo la Ubungo (Chadema) Mh. Boniface Jacob ameelezea mafanikio ya vielelezo vya mashtaka aliyopeleka Tume ya Maadili kuhusu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam yenye jumla ya makosa matano.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam meya huyo amesema kuwa siku ya Machi 22 mwaka huu, alipeleka rasmi mashtaka ya kumshtaki kiongozi huyo kuhusu kughushi vyeti, kula kiapo cha utii kwa rais, matumizi mabaya ya madaraka na kujipatia mali kwa njia zisizo sahihi.
Ameongeza kuwa pamoja na mashtaka hayo, aliwasilisha vielelezo vya majina yake, vyeti na wanafunzi aliosoma nao.
Aidha amesema kuwa Tume ya Maadili imeonyesha mwanzo mzuri ambapo imetoa majibu ya barua iliyopelekewa kuhusu malalamiko hayo na kero za mkuu huyo wa mkoa.