×

Wakati Mourinho Akimfanyia Figisu, Bastian Schweinsteiger Anyakuwa Tuzo Kwao Ujerumani

Kiungo wa Kimataifa wa Ujerumani anayechezea Man United ya England Bastian Schweinsteiger ameshinda tuzo ya heshima ‘Special Jury’ kwa mchango wake katika timu ya taifa ya Ujerumani, Bastian ameshinda tuzo hiyo licha ya kuwa katika kipindi kigumu chini ya Kocha wa Man U, Jose Mourinho kutompanga kwenye kikosi cha kwanza.

3a7d870f00000578-0-image-m-99_1479430639608Bastian Schweinsteiger

Bastian ambaye ametangazwa mshindi wa tuzo hiyo inayoandaliwa na vyombo vya habari vya Ujerumani na kujulikana kwa jina kama la Bambi Awards, ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo kwa ushirikiano wake, pamoja na kocha wao wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Low ameshinda tuzo kwa ushirikiano wake timu ya taifa.

3a7d2a3800000578-0-image-m-97_1479430590920Bastian na mkewe Ana Ivanovic

Kiungo huyo ambaye aliambatana na mkewe ambaye ni mchezaji tennis Ana Ivanovic, alitangaza kustaafu kucheza timu ya taifa ya Ujerumani mwezi August 2016, Bastian amefanikiwa kushinda kombe la dunia akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani mwaka 2014.

3a7e49ec00000578-0-image-a-92_1479429026040

Joachim Low