Manchester United wanaonolewa na Kocha asiyeishiwa maneno, Jose Mourinho waliyokuwa nyumbani kweye uwanja wao wa Old Trafford, wameshindwa kutamba mbele ya mahasimu wao Arsenal kwenye mechi ya Ligi Kuu England baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1.
Mechi hiyo iliyokuwa ikifuatiliwa na watu wengi sehemu mbalimbali dunian, imefanya mwendelezo wa matokeo ya Mourinho kikosini kwake kutokuwa ya kuridhisha kama watu wengi walivyokuwa wakitarajia wakati akitua kwa Mashetani Wekundu hao.
Katika mechi hiyo, kipindi chote cha kwanza timu zote zilienda mapumzikoni zikiwa sare ya bila kufungana, lakini baada ya kutoka mapumzikoni hali ilibadilika ghafla uwanjani huku kila timu ikifanya juhudi za hali na mali ili kuondoka na matokeo.
Wenyeji Manchester ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao, juan Mata kunako dakika ya 68 baada ya kumalizia crosi nzuri kutoka kwa Ander Herrera. Olivier Giroud aliisawazishia Arsenal kunako dakika ya 89 ya mchezo huo.



















Comments are closed.