MWANAMFALME wa Uingereza, Prince Harry amekutana na nyota wa muziki wa Pop duniani, Rihana mara mbili kwa siku katika hafla ya kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Barbados.
Rihana ambaye muziki wake unapendwa sana nchini Uingereea alisamama na kumsalimia Prince Harry. Kisha wawili hao wakaketi pamoja jukwaani wakati wa hafla hiyo.
Msaidizi mmoja alisema kuwa Prince Harry ambaye alivalia nguo rasmi za ufalme alisema kuwa Harrry alikuwa amejulishwa dakika 20 kabla ya kuanza kwa hafla hiyo kuwa Rihana angehudhuria. Baadaye Harry na Rihana tena waliketi pamoja kwenye jukwaa eneo la Kensington huko Bridgetown.
Umati wa watu 20,000 uliohudhuria ulimshangilia Prince Harry wakati jina lake lilipotajwa, Lakini kulikuwa na mbwembwe zaidi wakati jina la Rihana lilitajwa.

