×

Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco Atumbuliwa

mrambaaa

Mhandisi Felschemi Mramba

umeme

Taarifa kutoka Ikulu

Rais John Pombe Magufuli, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Felschemi Mramba kuanzia leo, Januari 1, 2017.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Gerson Msigwa, Rais Magufuli amemteua Dkt. Tito Esau Mwinuka kuwa kaimu mkurugenzi wa shirika hilo. Kabla ya uteuzi huo,  Mwinuka alikuwa Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).