
Mkali wa ngoma ya Inde, Dully Sykes, usiku wa Mwaka Mpya aliangusha shoo ya nguvu kwenye Ukumbi wa Maisha Basement, Makumbusho jijini Dar sambamba na mkali wa Ngoma ya Matatizo, Harmonize na Kundi la Makomandoo.
Mpango mzima ulianza mishale ya saa saba usiku, Januari 2, 2017 ambapo Makomandoo ndiyo waliofungua steji, wakaangusha shoo ya nguvu huku wakishangiliwa, wakafuatiwa na Dully Sykes ambaye aliwarusha mashabiki zake kwa ngoma kali kama Inde, Salome, Kariakoo na nyingine kibao.
Aliyefunga pazia alikuwa ni Harmonize ambaye usiku huo aliongozana na ‘usingizi’ wake, mwanadada Wolper anayefanya poa kwenye Bongo Movie, aliyekamua mpaka majogoo.
Na Hillaly Daudi/ GPL.