×

Mbeya Wachangamkia Shindano la Shinda Nyumba

shinda-nyummba-mbalizi-7  DERICK LWASYE,  Mbeya

SHINDANO la Shinda Nyumba na Global Publishers awamu ya pili, limepokelewa vizuri na wasomaji wa maga­zeti ya Global Publishers, kampuni namba moja ya uchapishaji wa magazeti Tanzania.

shinda-nyummba-mbalizi-4Hii ni mara ya pili kwa shindano hili la shinda ny­umba kufanyika, huku awa­mu ya kwanza akipatikana mshindi wa mjengo wenye thamani ya mamilioni kutoka mkoani Iringa, Nelly Mwangosi.

shinda-nyummba-mbalizi-9Wasomaji wa Mbalizi wakichangamkiaMagazeti ya Global Publishers ili kujaribu bahati yao ya Kushinda Nyumba.

Wakizungumza na Cham­pioni Jumatatu wakati wa promosheni ya shindano hilo iliyofanyika katika mae­neo mbalimbali ya viunga vya Jiji la Mbeya, wasomaji hao walisema wana uhakika na kile kinachofanywa na Global Publishers.

mwanjelwa-1“Siyo siri ninyi jamaa mko vizuri sana na hamna magu­mashi kwenye bahati nasibu zenu, hivyo nimejipanga ku­nunua kopi nyingi za maga­zeti ya Global Publishers ili nijitengenezee mazingira mazuri ya kuibuka mshin­di,” alisema Mussa Hassan ambaye ni Dereva Bajaji kwenye Kituo cha Kabwe.

mwanjelwa-2

Rodrick Robin, maarufu kama mzee wa Ijumaa Wik­ienda, alisema huu ndiyo wakati wa kujaribu bahati yake kutokana na kuwa mteja mzuri wa gazeti hilo ambalo huwa limesheheni hadithi zenye msisimko.mwanjelwa-3

Wakazi wa Mwanjelwa wakichangamkia Shinda Nyumba.

“Nimekuwa mteja wa muda mrefu wa maga­zeti ya Global Publishers ila nilikuwa sitilii maanani mashindano yaliyokuwa yakiendeshwa kutokana na kutoamini kama mshin­di anapatikana bila kupangwa, ila baada ya kuona mshindi wa awamu ya kwanza kapatikana kutoka Iringa, tena ni mwa­namke mjasiriamali, nikashawishika sana na sasa tutakula sa­hani moja mpaka kieleweke,” alisema Robin.

Katika eneo la Nanenane ambapo ndiyo kuna stendi ya mabasi ya wilayani na mikoani, waso­maji wa magazeti ya Global Publishers wal­ionekana kufurahia awamu hii ya pili ya Shinda Nyumba na Global Publishers.

Kwa upande wao wauza magazeti wa Jiji la Mbeya na nyanda za juu kwa ujumla, wamewa­taka mawakala wa magazeti ya Global Publishers kuagiza nakala nyingi ili kue­pusha usumbufu kama ulivyojitokeza awamu ya kwanza ya shindano hili.

“Unajua shindano hili ni kubwa sana hapa Tanzania, hivyo kila mtu atataka kujari­bu bahati yake, tunawaomba mawakala wajitahidi kuagiza nakala za kutosha ili kuwaon­dolea usumbufu wasomaji na wateja wetu, msimu uli­opita kulikuwa na uhaba wa nakala, hivyo kuna baadhi ya wasomaji walikuwa wanako­sa nakala.”

Maeneo mengine ambayo promosheni hiyo ilifanyika ni Mbalizi, Uyole, Mwanjelwa, Soweto, Iyunga na Sokoma­tola.