×

PICHAZ 24: Gwajima, Manji Walivyochukuliwa Kituo Kikuu cha Polisi na Kupelekwa Kusikojulikana

Baada ya Askofu Gwajima na Mwenyekiti wa Yanga na Mfanyabiashara Yusuph Manji kuwasili kituo cha kati cha Polisi Dar es Salaam na kukaa zaidi ya saa zaidi ya 5, wameondolewa kwenye eneo hilo.

Gwajima na Manji wamepakizwa kwenye gari moja na kuelekea sehemu ambayo kamishina wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Simon Sirro hakutaka kuweka wazi lakini akawaambia Waandishi wa habari waliokua nje ya kituo kuwa taarifa rasmi atazitoa kesho Ijumaa ya February 10 2017.