
MKUU wa Chuo cha Maji (Water Institute) kilichoko jijini Dar es Salaam, Shija Kazumba, ameziomba mamlaka za serikali na taasisi kutumia au kuwaajiri wataalam wa maji wanaomaliza masomo yao kutoka chuo hicho katika shughuli nzima za miundombinu ya maji hadi katika uhifadhi bora wa maji.

Hayo ameyasema leo alipozungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, alipofafanua kwamba chuo chake hadi sasa kina wanafunzi 1,849 kati yao wanawake wakiwa 489 hivyo akaomba taasisi na mamlaka mbalimbali kuwatumia wataalam wanaotoka katika chuo hicho kwani tayari wanakuwa wamepata elimu ya kutosha kuhusiana na masuala ya maji kwa jumla.

Alisisitiza kwamba wahitimu wa chuo hicho wote ni bora akimaanisha wanaume na wanawake ambapo wanaweza kufanya kazi zote zinazohusiana na miundombinu ya maji kikamilifu.
Na Denis Mtima/GPL