×

Frank Mgogosi Aibuka Mshindi wa Wikienda Music Search

Mshiriki Allen Venance akiwa mbele ya majaji

MSANII wa Bongo Fleva, Frank Mgogosi mkazi wa Kimara jijini Dar jana ameibuka Mshindi wa Shindano la Wikienda Music Search (WMS) lililoandaliwa na Gazeti la Ijumaa Wikienda la ‘Unataka Kuwa Msanii Mkubwa wa Muziki’.

Mshindi wa Shindano la Wikienda Music Search (WMS, Frank Mgogosi

Fainali ya shindano hili lilifanyika kwenye Studio za Wanene Entertainment zilizopo Mikocheni jijini Dar chini ya maproduzya watano akiwemo King Luffa, Dk, Reggy, Goncher, Humphrey kutoka zimbambwe na Shente Murozy wa Studio za Black za Magomeni Kagera jijini Dar.

Mmoja wa wafanyakazi wa Wanene Entertainment, Glady akifuatilia usahili

Akizungumza na GPL, Mgogosi ambaye ni mshindi ameyapongeza Magazeti ya Global Publishers kwa kutoa fursa mbalimbali kwa wasomaji na wasanii na kuwahimiza Watanzania kuwa na utamaduni wa kujisomea.

…Allen akionesha uwezo wake mbele ya majaji

“Sikutegemea kama naweza kuwa mshindi maana hata mpinzani wangu Allen Venance yuko vizuri lakini kwa kuwa mshindi alipaswa awe mmoja, nimepita mimi.

Washiriki wakiwa mbele ya majaji

“Niwashauri tu Watanzania na hasa vijana wajenge utamaduni wa kujisomea hasa Magazeti ya Global kwani kuna habari zingine ambazo zinaweza kuwa fursa kwako, alisema Mgogosi.

Mratibu wa WMS, Gabriel Ng`osha akiwa na washiriki siku ya fainali

Aidha Mratibu wa Shindano la Wikienda Music Search (WMS), Gabriel Ng’osha amewapongeza wasanii zaidi ya 60 waliojitokeza kwa jiji la Dar e s Salaam na kuwataka kuendelea kusoma Gazeti la Ijumaa Wikienda, kwani limejipanga kuboresha zaidi Shindano hilo.

 

Mtayarishaji wa muziki, King Lufa akitangaza matokea

Mtayarishaji Shente Murozi akitoa nasaha zake

Na mwandishi wetu/GPL