×

Meya wa Jiji la Dar Aipiga Tafu Shule ya Msingi Mji Mwema

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akizungumza jambo katika hafla hiyo.

MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita ameipiga tafu Shule ya Msingi Mji mwema iliyopo Wilaya ya Kigamboni kwa kuchangia saruji mifuko 100 na mabati 100 kwa ajili ya upanuzi wa vyumba vya madarasa ya shule hiyo.

Taswira ya hafla hiyo ilivyoonekana katika Shule ya Msingi Mji Mwema.

Hafla ya uchangiaji wa mifuko hiyo, ulifanyika katika shule hiyo ambapo pia kulihudhuriwa na diwani wa kata, Celestine Maufu, walimu,wadau na wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo, ambao walionekana kufurahishwa na namna meya alivyojitolea kufanikisha ujenzi.

Diwani wa Kata ya Mji Mwema Kigamboni,Celestine Maufu (aliyesimamakushoto) akitoa ahadi yake ya mchango.

Hafla hiyo ilikuwa ya harambee ya uchangiaji fedha kwa ajili ya upanuzi wa vyumba vya madarasa, ambapo katika hotuba yake mwenyekiti wa kamati ya shule alisema kuwa madawati yapo lakini tatizo ni sehemu ya kuyaweka.

Meza kuu ilivyoonekana.

 

Shughuli za utoaji ahadi zamichango ukiendelea.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo ya harambee ya uchangiaji fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

NA DENIS MTIMA/GPL