×

WAWILI WAONDOKA NA BODABODA SHIKA NDINGA YA EFM

Meneja Mkuu wa Redio Efm na Tv E, Dennis Ssebo, akizungumza kabla ya kukabidhi kadi kwa washindi wa pikipiki wa Shindano la Shika Ndinga wa mkoa wa Dar es Salaam.

 

WAKAZI  wawili wa Dar es salaam, Ashura Ramadhan na Abbas Awadhi waliibuka kidedea baada ya kuwa  washindi katika shindano la shika ndinga linaloendeshwa na kituo cha Redio cha Efm na Tv E.

Washiriki wa shindano la Shika ndinga kwa Mkoa wa Dar es Salaam wakichuana wakati wa shindano hilo lililofanyika katika Viwanja vya Mwembeyanga.

Ashura Ramadhan mkazi wa Bunju  alipiga simu na kupata nafasi hiyo kupitia kipindi cha uhondo ambapo mshindi mwingine ni Abbas Awadhi, ambaye ni mkazi wa Mwananyamala aliyeshiriki shindano hilo kupitia kipindi cha Genge kinachoendeshwa na kituo hicho cha redio. Hafla ya kuwapata washindi hao ilifanyika  siku ya Jumamosi katika Viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi za washindi hao Meneja Mkuu wa  Efm na Tv E, Dennis Busulwa alisema kuwa washindi hao wameshinda pikipiki na kupatiwa tiketi ya kushiriki fainali za shika ndinga zitakazo fanyika Dar es Salaam mara baada ya kuwapata washindi wa mikoani.

Mshindi wa Shindano la Shika Ndinga kwa Wanawake, Ashura Ramadhani mkazi wa Bunju akiwa juu ya pikipiki yake mara baada ya kukabidhiwa na Efm. 

Busulwa akikabidhi pikipiki hizo alisesema kuwa siku ya jumatatu (jana) washindi hao watafika katika ofisi za Efm na Tv E kwa ajili ya kubadilisha majina ya kadi za pikipiki hizo kutoka jina la kampuni kwenda majina yao.

Mshindi wa Shindano la shika ndinga  kwa upande wa wanaume, Abbas Awadhi ambaye ni mkazi wa Mwananyamala akiwa juu ya Pikipiki. 

Washindi hao walipatikana siku ya jumamosi kupitia mchakato  ulioanza asubuhi kwa mbio za kukimbia na vikombe vya maji kisha kufikia hatua ya pili ya kukimbia na mayai ambayo iliwapeleka kufika katika fainali na kuibuka kidedea.