×

KARIUS AOMBA MSAMAHA LIVERPOOL

KIPA wa Liv­erpool, Loris Karius, ame­waomba wenzake msamaha baada ya kufanya makosa k w e n y e mchez o wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

 

Kipa huyo alifan­ya makosa ya ma­bao mawili kwenye mchezo huo, bao la kwanza lililofungwa na Karim Benzema na bao la tatu lilo­fungwa na Gareth Bale, na jana alitua England akiwa ameficha uso wake kwa aibu.

 

Liverpool kwenye mchezo huo ulio­pigwa Kiev nchini Ukraine, walichapwa 3-1 na malalamiko ya mashabiki wa timu hiyo yameangukia kwa kipa huyo raia wa Ujerumani, ambaye hata hivyo wache­zaji wenzake waliko­solewa kumtenga wal­ipomuacha peke yake akilia baada ya kipyenga cha mwisho, aka­onekana akifari­jiwa na wache­zaji wa Real Madrid tu.

 

“Nimeisaba­bisha timu yan­gu ikakosa ub­ingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, napen­da kumuom­ba msamaha kila mmoja kwenye timu ya Liverpool.

 

 

“Sijisikii vizuri leo, nimewaan­gusha wenzangu, na­jisikia vibaya sana, nafikiri makosa yangu ndiyo yamesababisha timu ipoteze ubingwa.

 

“Ni siku mbaya kwangu, lakini haya ndiyo maisha ya mak­ipa, unaweza kufanya makosa na lazima ua­mke na kupambana tena,” alisema Mjeru­mani huyo.

 

Liverpool walitua nchini England mape­ma jana asubuhi huku wachezaji wakiwa na huzuni.

LIVERPOOL, England