×

NDONDO CUP YAANZA KUTIMUA VUMBI, DCB BENKI YANOGESHA – PICHAZ

Balozi wa DCB Benki, Nikki wa Pili (kushoto) akimsalimia mchezaji Totenham Hotspurs ya Uingereza, Victor Wanyama.

Michuano ya timu za mitaani maarufu kama Ndondo CUP jana ilizinduliwa rasmi kwenye Uwanja wa Kinesi uliopo Ubungo Shekilango Jijini Dar ambapo sasa pamoja na wadhamini wengine utadhaminiwa pia na Benki ya DCB kupitia huduma yao mpya ya Digital Account.

Baada ya kumsalimia Wanyama, Nikk aliwapa ‘hi’ na wadau wengine.

Akizungumza balozi wa DCB Benki ambaye ni mwanamuziki wa kizazi kipya kutoka Kundi la Weusi, Nikki wa Pili amesema wameamua kuidhamini michuano hiyo kutokana na kuwavutia watu wa kipato cha kati na cha chini ambao ambao wanaendana na huduma za kibenki wanazotoa.

Kikosi cha Keko Fenicha.

Nikki alisema benki hiyo inawahudumia hata wateja wenye kipato kidogo kabisa ambapo alisema wanaweza kufungua akaunti kwa Shilingi 5000/=.

 

Mabibo Market.

 

Katika funguzi huo timu za Mabibo Market na Keko Fenicha zilioneshana umwamba ambapo mpaka mwisho wa mchezo Mabibo Market ilichapa Keko Fenicha kwa mabao 3-2.

Wanyama akimsalimia mmoja wa wachezaji wa Keko Fenicha huku Balozi wa BCB Benki, Nikki wa Pili naye akifuatia.

Katika uzinduzi huo kama kawaida ya michuano hiyo vituko vilitawala mwanzo mwisho.

Meneja Masoko wa DCB Benki, Boyd Mwaisame (kulia) naye akikagua timu.
Moja ya patashika zilizotokea langoni mwa Keko Fenicha.

 

Mashabiki wa Keko Fenicha wakifanya vimbwanga. Shabiki wa Keko Fenicha akiwa amejipaka rangi mwilini.  

Wachezaji wa Mabibo Market wakishangilia bao la pili.

 

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS/GPL