×

Shinda Tiketi ya Kwenda Marekani na Kurudi Bure

Baraza la Watanzania Wanaoishi Nchi za Nje (DICOTA) wanakushukuru kwa kukubali kushiriki katika utafiti huu muhimu kuhusu ufahamu wa Watanzania wanaoishi nchi zanje (diaspora). Utafiti huu utasaidia kuwaeleza Watanzania walio nje sera za nchi hii.

 

Utafiti huu umeanza Juni 1 hadi Julai 12, 2018 na utachukua dakika tano hadi saba tu kukamilika. Uwe na uhakika kwamba majibu yako yatakuwa ya siri na hayatakuwa na jina lako.

Utapata fursa ya kujiunga na kushinda tiketi ya kwenda na kurudi kwenye mkutano wa Baraza la Watanzania Wanaoishi Nchi za Nje (DICOTA) wa 2018 utakaofanyika huko Seattle, Washington, na kupata msamaha wa kodi wa DICOTA Convention Registration Fee Waiver, simuzai-pads na Kadi za Zawadi.

 

DICOTA limedhamiria kuendeleza maisha ya kijamii na kiuchumi ya Tanzania na Marekani. Lengo lake kuu ni kubadilishana dhana mbalimbali, ufanyajikazi bora zaidi na mijadala na wakala baina yaserikali na taasisi, nakuhakikisha kuwa kichocheo cha kuanzishwa kwa ushirikiano bora zaidi wa kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kati ya Marekani na Tanzania.

 

Inakadiriwa kuna Watanzania milioni tatu wanaoishi nchi zanje. Wizaraya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inakadiria kwamba Watanzania wanaoishi nje huingiza wastani wa Dola mil. 457 (Shtril. 1.03) kila mwaka.

 

DICOTA inaaminikikamilifukatika Tanzania ya kidemokrasia, isiyoendeshwa kidini, inayoendeleza utamaduni wake na yenye kujijenga kiuchumi. DICOTA ni shirika huru, lisilofungamana na upande wowote, lisilokuwa la kidini, lenye dhamira ya kuendeleza ufahamu kuhusu Tanzania na ukuaji wake wakiuchumi.

 

Shirika hilo linategemea kuwa sauti ya kuaminika, yenye busara na huru kwa Tanzania. Kwa kupitia kazi zake, DICOTA itakuwa chanzo cha mazungumzo muhimu na kichocheo cha mabadiliko chanya nchini Tanzania, na itatoa sauti yake katika mijadala mbalimbali nchini Marekani juu ya masuala yanayoihusu Tanzania.

 

Nia ya DICOTA ni kuunganisha na kuwaimarisha Watanzania walioko Marekani na wafuasi wake ili kuwaendeleza kiuchumi, kiafya na kijamii Watanzania naWamarekani.

Diaspora Council of Tanzanians in America (DICOTA) ni shirikalisilo la kibiashara, lililosamehewa kulipa kodi kwa mujibu wa kifungo cha 501 c (3) Tax Exemption Status.

Kushinda tiketi ya kwenda Marekani na kurudi bure bofya hapa ===> http://dicotaus.org/who-we-are.php