×

Breaking News: Kangi Lugola Awatumbua Vigogo Wawili

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akisalimiana na Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya, Mratibu wa Polisi, Leopard Fungu, baada ya kuwasili jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi juzi.

 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ametoa agizo kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, kumshusha cheo Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya, Leopold Fungu.

Lugola ametoa agizo hilo leo Julai 6 wakati akifanya cha kimkakati cha viongozi wa vyombo na taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo, ambapo ameagiza RTO Fungu ashushwe cheo hadi kubaki na nyota tatu.

 

Aidha, Lugola ameagiza Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto mkoa wa Kagera, George Mrutu ashushwe cheo.

MUNA AZIMIA! Mapokezi ya PATRICK Airport