Mbunge wa Tarime vijijini, John Heche, amehoji Bungeni sababu ya Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli kuharakisha mchakato wa kuwahamishia watumishi wa umma Dodoma bila kuwapatia stahiki zao huku ikijua inafanya makosa.
Heche amesema hayo wakati akichangia mapendekezo yake katika muswada wa sheria ya kulifanya jiji la Dodoma kuwa makao makuu.