×

Breaking: Ibrahim Ajib Aikacha Yanga, Atambulishwa Simba

Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajib akisani mkataba wa miaka miwili Simba.
…Akiweka pozi baada ya kusani mkataba.
Mkurugenzi Mtendaji (C.E.O) wa klabu ya Simba, Crescentius Magori (kushoto) akimpa mkono wa kumkaribisha Ibrahim Ajib.

Klabu ya Simba imetangaza kumsajili kiungo mshambuliaji, Ibrahim Ajib kwa mkataba wa miaka miwili kutoka klabu ya Yanga.

Ajibu msimu wa 2018-19 alikuwa kwenye ubora wake baada ya kutoa jumla ya pasi za mabao 17 na kufunga mabao sita.

Ajibu alijiunga na Yanga msimu wa 2017-18 akitokea Simba na amecheza misimu miwili bila kutwaa kombe akiwa na Yanga sasa amerejea rasmi kwenye klabu yake ya zamani ya Simba.