
Kampuni ya Simu za mkononi ya Vodacom jana ilizindua simu mpya inayokwenda kwa jina la Smarti Kitochi. Akizungumza na wanahabari kwenye duka la Vocacom Mlimani City Dar, Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Mawasiliano wa kampuni hiyo, George Lugeta amesema simu hiyo wameipa jina hilo kutokana na uwezo wake mkubwa unaofanana na smart phone. Lugata amesema simu hiyo ina spidi ya aina yake katika matumizi ya data ikiwa Whatsapp, Facebook, Twitter, na mitandao mingine.


HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS NA NEEMA ADRIAN/GPL