×

Feza Kessy Ashangazwa na Ali Kamwe “Aliomba Namba, Kisha Akapotea!”

Msanii wa Bongo Flava, Feza Kessy

Msanii wa Bongo Flava, Feza Kessy, ameeleza kushangazwa na kitendo cha Afisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, kumuomba namba ya simu lakini kisha kutowasiliana naye tena.

Katika mahojiano ya hivi karibuni, Feza alisema tukio hilo lilitokea wakati wa sherehe ya harusi ya Hamisa Mobetto na Aziz Ki huko Masaki.

Afisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe.

Kwa mujibu wa Feza, Kamwe alimfuata na kuomba namba yake ya simu, akaiandika mwenyewe kisha akamwambia aihifadhi kama “Feza”. Hata hivyo, tangu siku hiyo, hakuna mawasiliano yoyote yaliyofuata.

“Sielewi ilikuwaje! Aliniomba namba, akaandika mwenyewe, akasema nisave Feza, lakini baada ya hapo—kimya!” alisema Feza kwa mshangao.

… Ali Kamwe akisave namba ya Feza