×

Mvutano wa Israel na Hamas Wazidi: Israel Yatuhumu Hamas kwa Propaganda

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu

Israel imesema kuwa kundi la Hamas halijabadilisha msimamo wake katika mazungumzo ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza na kinachofanyika ni “vita vya propaganda.”

Kwa mujibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ingawa Israel imekubali muundo wa mpatanishi wa Marekani kwa Mashariki ya Kati, Steve Witkoff, Hamas bado inashikilia msimamo wake wa awali. Israel imekishutumu kundi hilo kwa kutumia hujuma na propaganda katika mgogoro huo.

Wakati huo huo, Hamas imetangaza kuwa itamuachia huru raia mmoja mwenye uraia wa Marekani na Israel aliyetekwa nyara katika Ukanda wa Gaza. Kundi hilo pia limesema lipo tayari kuikabidhi miili ya mateka wengine wanne wenye uraia wa mataifa mawili, ingawa halijataja uraia mwingine wa Waisraeli hao waliokufa.

Hatua hiyo inadaiwa kuchukuliwa kufuatia pendekezo la wasuluhishi wa mgogoro huo. Hata hivyo, tarehe ya kuikabidhi miili hiyo bado haijabainishwa.