×

Dili la Moto! Aziz Ki Apiga Jackpot ya Bilioni Morocco

Stephene Aziz Ki

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga raia wa Burkina Fasso, Stephene Aziz Ki anatajwa kuingia kwenye orodha ya wachezaji wanaokuja mkwanja mrefu kutokana na thamani yake kuendelea kupaa juu.

Nyota huyo kwa sasa hatakuwa ndani ya kikosi cha Yanga SC msimu wa 2025/26 baada ya kupata changamoto mpya nchini Morocco ambapo amepata dili jipya.

Taarifa zinaeleza kuwa nyota huyo kwenye upande wa mkwanja atakuwa anakunja Sh 1.2Bil kwa mwaka kama sehemu yake ya mshahara hiyo ni kuweka kando mkwanja wake wa usajili ambao amevuta mezani.

Aziz Ki ni dili la miaka miwili amesaini Wydad Athltic Club huku ikielezwa kuwa atakuwa analipwa mshahara wa zaidi ya milioni 88 kwa mwezi, ambao utamfanya akunje zaidi ya bilioni kwa mwaka.

Ikumbukwe kwamba kutakuwa na bonasi ambazo atakuwa anakuja Aziz jambo litakalomfanya awe anavuta mkwanja mrefu kwa mwaka.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.