
Kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi WCF Julai 1, 2025, WCF imetoa Mafunzo kwa Wadau wa Mfuko huo ya usalama na afya mahala pa kazi na kutoa elimu kuhusiana na uwasilishaji wa madai ya fidia kwa njia ya mtandao.
Mafunzo hayo yamefanyika Jijini Dar es Salaam yakiwa yamewalenga Watumishi kutoka Sekta binafsi na ile ya Umma.
Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini- WCF, Dk. Abdulsalaam Omar amesema wanatumia nafasi hiyo pia kuwaelimisha wadau shughuli mbalimbali ambazo zinafanywa na WCF ikiwemo mafao ya fidia kwa wafanyakazi yanayotolewa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).

‘‘Katika siku hii tuna wadau mbalimbali ambao ni wawakilishi wa waajiri wakiwemo maafisa Rasilimali watu, Maafisa usalama na Afya Mahala Pa kazi na tunakutana nao hapa kwaajili ya kubadilishana mawazo, kukumbushana namna ya kubaini vihatarishi katika maeneo yao ya kazi lakini pale ambapo ajali au magonjwa yanapokuwa yanatokea ni namna gani ya kuweza kuwasilisha madai mapema, lakini pia tunataka kupeana uelewa wa namna ya kuweza kufanya uchunguzi wa ajali zinazotokana na kazi na namna bora ya kuweza kudhibiti hizo ajali’’ amesisitiza Dk. Omar

‘‘Kwahiyo kupitia program hii na sisi tumepatiwa elimu kiwandani kwetu kwani tulipata mafunzo ambayo tunaendelea kufanyia kazi. Miaka 10 ya WCF sisi tunashukuru mfuko huu kuendelea kutufikia na kutuhudumia” ameongeza Shebuge



WCF imeendesha mafunzo hayo ikiwa na lengo la kuendelea kuwapa uelewa kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko huo, Usalama na Afya Mahala Pa Kazi, Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi na Hatua za kufuata wakati wa kuwasilisha Madai ya Fidia kwa Wafanyakazi hususani kuwasilisha madai kwa njia ya mtandao.





