
Droo ya hatua ya awali (preliminary round) ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu wa 2025/26 imekamilika ambapo wawakilishi wa Tanzania kwenye CAFCL, Simba Sc, Yanga Sc na Mlandege Fc wamebaini wapinzani wao kwenye ‘CAFCL Preliminary round’
Mabingwa wa Ligi Kuu bara Yanga Sc wamepangwa dhidi ya vigogo wa Angola, Wiliete Benguela Sc huku watani zao Simba Sc wakikutanishwa na wababe wa Botswana, Gaborone United wakati Mlandege Fc ikipewa Ethiopia Insurance ya Nchini Ethiopia.
Eth. Insurance 🇪🇹 🆚 Mlandege (Znz)
Gaborone Utd 🇧🇼 🆚 🇹🇿 Simba Sc
Wiliete Benguela 🇦🇴 🆚 🇹🇿 Yanga Sc