The House of Favourite Newspapers

Uchaguzi Zimbabwe: Mataifa Yaitolea Tamko Zimbabwe Ikomeshe Vurugu

Matumizi ya nguvu ya serikali dhidi ya upinzani nchini Zibabwe baada ya uchaguzi wa Jumatatu yameichochea jamii ya kimataifa kutoa wito wa kumaliza vurugu.

 

Umoja wa mataifa na Umoja wa Ulaya kwa pamoja wamekemea juu vurugu zilizotokea na polisi kufyatua risasi kwa waandamanaji.

 

Makundi ya waandamanaji yalikuwa katikati ya mji huo tangu alfajiri lakini habari zilipozuka kwamba Zanu PF imeshinda viti vingi katika bunge na kwamba matokeo ya urais hayakuwa tayari, hali ilibadilika.

Lakini upinzani wanasema kuwa ZANU PF imeingilia uchaguzi.

Uchaguzi wa Jumatatu ulivutia asilimia 70 ya wapiga kura. Chombo cha habari cha ZBC kimesema kuwa Zec itatangaza matokeo ya uchaguzi wa urais mwendo wa 12.30 za Zimbabwe.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa serikali ya Zimbabwe inatakiwa kuhakikisha kuwa vurugu hizo hazitokei.

 

Wakati huo huo shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International linaitaka serikali kufungua mashataka kwa polisi waliofyatua risasi kwa waandamanaji.

”Vikosi vya usalama vinapoingilia uchaguzi ni kuwanyima haki wananchi ya kujieleza,” amesema katibu wa Amnesty.


Ni matokeo gani ambayo yametangazwa hadi sasa?

Tume ya uchaguzi ya Zimbabwe(Zec) hadi sasa imetangaza ushindi wa viti 140 kwa chama tawala cha Zanu-PF, huku kile cha Muungano wa Upinzani MDC kikiwa na viti 58 , kulingana na taarifa ya Shirika la Utangazaji la taifa ZBC . Kuna viti 210 Katika Bunge la Taifa.

Zaidi ya watu milioni tano walijiandikisha kupiga kura, na watu wengi walijitokeza kushiriki uchaguzi kwa kiwango cha 70%.

Ni nini wanachosema wakaguzi wa uchaguzi?

  • Muungano wa Ulaya umekosoa kuchelewa kutangazwa kwa matokeo ya urais.
  • Umesema kuwa ilibaini baadhi ya matatizo, ukiwemo upendeleo wa vyombo vya habari, vitisho kwa wapiga kura na kutokuwa na imani na tume ya uchaguzi , ukiongeza kuwa ”mazingira ya uchaguzi hayakuboreshwa na hivyo kusababisha kuwepo kwa hali ya kiwango kikubwa cha ukosefu wa uaminifu “.
  • Hii ni mara ya baada ya miaka 16 kwa serikali kuwaruhusu waangalizi wa uchaguzi kutoka Muungano wa Ulaya na Marekani kuchunguza uchaguzi
  • Kwa upande wa Muungano wa Afrika, mapema wiki hii umesema kuwa uchagauzi huo ulikuwa huru na wa haki , akiongezea kuwa unaadhimisha wakati muhimu wa mabadiliko ya kisiasa.
  • Ripoti ya awali kutoka waangalizi wa SADC inasema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa amani na ulifanyika kulingana na sheria.
  • Wawakilishi wake, waziri wa maswala ya kigeni nchini Angola Manuel Domingos Augusto ameutaja uchaguzi huo kuwa kidemokrasia.
  • Muungano wa Comesa ulisifu tume ya uchaguzi kwa kutumia kifaa cha Biometric kusajili wapiga kura akisema kuwa kimepunguza uwezekano wa watu kupiga kura zaidi ya mara moja.

CHANZO: BBC SWAHILI

Comments are closed.