×

Tiwa Savage Arudiana Kimya Kimya na Mumewe Teja wa Madawa Teebillz

vllkyt192shj5o9fog-ed78af29

NIGERIA: MWANADADA maarufu kwenye tasnia ya muziki Barabi Afrika, Tiwa Savage amerudiana na mumewe Teebillz baada ya kuachana naye kwa kile kilichodaiwa kuwa mwanamme huyo anatumia madawa ya kulevya.

Imeelezwa kuwa, Teebillz  amefanikiwa kutibiwa kisiri katika kliniki ya tiba ya madhara yatokanayo na matumizi ya madawa ya kulevya pamoja na kufanyiwa ushauri wa masuala ya ndoa (Drug Addiction Rehabilitation & Series Of Marriage Counselling).

tiwa-2Kwa mujibu wa televisheni moja ya nchini Nigeria humo iliyomfanyia mahojiano Tiwa, imeeleza kuwa amerudiana na mumewe huyo kimya kimya bila watu kujua kwa kile alichokieleza kuwa afya ya mumewe huyo inaendelea kuimarika baada ya kutibiwa utumiaji wa madawa ya kulevya uliokuwa umemuathiri kwa kiwango kikubwa, mbali na afya yake kuimarika, sababu nyingine ni kwamba wawili hao wanataka wamlee kwa pamoja mtoto wao wa kiume aitwae Ajmil.

tiwa-savageJapo bado wapo kwenye harakati za mwanzo kurudiana pole pole, huku uhusiano wao ukionekana kuanza kuimarika upya siku hadi siku, wawili hao wamekuwa wakionekana kwa pamoja wakienda kwenye kituo kimoja cha ushauri wa masuala ya kisaikolojia na mambo ya ndoa jijini Lagos kwa ajili ya kupata ushauri nasaha kuhusu ndoa yao.

 halotel-strip-1-1

MZEE WA MIAKA 76 ALEYETANAGAZA KUTAFUTA MKE “FULL EXLUSIVE INTERVIEW”