
Mashabiki waliokuwa wamefurika kwenye Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live kwenye mkesha wa mwaka mpya kulipokuwa na shoo kali ya Nichane Nikuchane ambapo miamba miwili, Roma na Darassa ilioneshana kazi, walipata fursa ya kipekee ya kuupokea mwaka wakiwa ndani ya ukumbi huo na kuandika historia ya kipekee ya kuuanza 2017 wakiwa ukumbini hapo. Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio yaliyotokea dakika chache kabla ya kutimu saa sita kamili za usiku, ilipotimu na yaliyoendelea baada ya kuuona mwaka mpya. Ilikuwa poa sana!