
WASANII wawili wa Muziki wa Bongo Fleva, wamefanikiwa kuingia kwenye fainali ya Shindano la Wikienda Music Search (WMS) linaloendeshwa na Gazeti la Ijumaa Wikienda baada ya kupita kwenye mchujo uliofanyika leo kwenye Studio za Black zilizopo Magomeni- Kagera jijini Dar.

Wasanii hao ni Alen Venance kutoka Ilala na Frank Mgogosi wa Kimara ambao wamewamwaga wasanii wenzao 18 akiwemo mwanadada mmoja.







Washindi hao wawili watapambana hivi karibuni kwenye Studio za Wanene Entertainment zilizopo Mwenge jijini Dar.
Mratibu wa WMS, Gabriel Ng’osha, amewashauri wasanii wa kike kujitokeza kwa wingi zinapotokea fursa za sanaa, ujasirimali na nyinginezo, ili kuweza kufikia ndoto zao kwani hakuna anayefahamu atafanikiwa kwa njia gani.
Shindano hili limeandaliwa na Gazeti la Ijumaa Wikienda na kudhaminiwa na Studio ya Black na Wanene Entertainment.
Habari/Picha:Gabriel Ng’osha/GPL