Msanii Suma G akizungumza na Global TV msibani hapo.
JUZI JUMATANO, Mei 17, 2017 tasnia ya muziki wa Bongo ilikumbwa na msiba mkubwa baada ya kuondokewa na msanii Mfaume Suleiman ‘Dogo Mfaume’ aliepata umaarufu kutokana na wimbo wake wa ‘Kazi ya dukani’, mauti yalimkuta akiwa kwenye hospitali ya taifa Muhimbili akijiandaa kufanyiwa upasuaji kichwani ambapo amezikwa leo Mei 19 katika makaburi ya Chanika jijini Dar es salaam.
Mwili wa marehemu ukitolewa ndani
Shughuli ya kuuzika mwili wa marehemu Dogo Mfaume imefanyika nyumbani kwao Chanika ambapo amezikwa katika makaburi ya Kwa Mbiki – Chanika jijini Dar es Salaam.
Jeneza lenye mwili wa marehemu
Mwili wa marehemu ukielekea makaburi ya Kwa Mbiki – Chanika tayari kwa maziko.Waombolezaji wakiuswalia mwili wa marehemu kabla ya maziko, katikati wenye kanzu ni Mzee Yusuf.
Shughuli ya kuuhifadhi mwili wa marehemu Dogo Mfaume.
Waathirika wa dawa za kulevya kutoma Pili Foundation (Soba) wakimwombea dua marehemu Dogo Mfaume.
Inspekta Horoun (mwenye kanzu nyeupe ) akiwa na waombolezaji wengine ndani ya kaburi tayari kumzika marehemu Dogo Mfaume.