The House of Favourite Newspapers

Amber Lulu Awafungukia Wanaomponda

0
Lulu Augen ‘Amber Lulu’.

Lulu Augen ‘Amber Lulu’ amefungukia lawama ambazo amekuwa akizipata sababu ya

vituko anavyovifanya katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuwa anafanya hivyo kwa kuwa mwezi huu hauendani na imani yake.

Akibonga machache na Star Mix, Amber ambaye amekuwa akiachia video mitandaoni akicheza kihasara katika kipindi hiki alisema, anawashangaa wanaomponda na kumtaka ajiheshimu kuwa waache kufuatilia maisha yake.

“Nawashangaa wanaokaa kunifuatilia eti nijiheshimu. Sioni kama nina kosa katika huu mwezi kwa maana mimi ni Mkristo hivyo

nitaendelea kufanya kitu roho inapenda, wasifuatilie maisha yangu,” alisema.

 

Leave A Reply