The House of Favourite Newspapers

Halima Azidi Kuisakama Serikali Hoja za Kuporomoka kwa Uchumi

0
Mbunge Halima Mdee.

Waziri Kivuli wa Mipango, Fedha na Uchumi, Halima Mdee ameitaka Serikali kujibu hoja kuhusu kuporomoka kwa uchumi katika utawala wa Rais John Magufuli badala ya kuwadanganya wananchi.

Mdee ambaye pia ni mbunge wa Kawe (Chadema) amesema hoja zilizotolewa na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe hazijajibiwa na Msemaji wa Serikali, Dk Hussein Abbas badala yake anatoa takwimu za uongo.

 

Amebainisha hoja mbalimbali zinazohitaji majibu kuwa ni Serikali kueleza kwanini kilimo kimeporomoka na itoe mpango mkakati wa kuinua kilimo nchini.

Pia, amehoji kushuka kwa uchumi wa benki ambazo hazitoi mikopo kwa wafanyabiashara.

“Tulichokuwa tunakizungumza juzi ndiyo hicho wamekizungumza jana watu wa TPSF. Serikali imeondoa fedha zake kwenye benki za biashara na kwenda kuzifungia BOT. Huku kwenye mzunguko hakuna hela,” amesema.

 

Hata hivyo, Mdee amesema katika bajeti ya mwaka 2017/18, Serikali inatarajia kukopa Sh7 trilioni, mkopo wa ndani ukiwa ni Sh6 trilioni na mkopo wa nje Sh1 trilioni.

“Serikali hii ambayo haizisaidii benki zake zichanue, ndiyo hiyo hiyo inategemea kukopa Sh6 trilioni kwenye benki hizo hizo,” amesema Mdee.

 

HALIMA MDEE AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI

Leave A Reply