×

Moto Wateketeza Soko la Sido Mbeya (Video)

Moto ukiendelea kuwaka kwa kasi kwenye Soko la Sido lililopo mkabala na maeneo ya Mwanjelwa jijini Mbeya.

Usiku wa kuamkia leo Soko Kuu la Jijini Mbeya maarufu kama SIDO, lililopo mkabala na maeneo ya Mwanjelwa jijini Mbeya linateketea kwa moto  chanzo cha moto huo bado hakijajulikana mpaka sasa.

Moto ukiteketeza soko hilo.

 

Moto ukiteketeza soko hilo.

Moto huo ulianza kuwaka mnamo majira ya saa tatu usiku na kusababisha tafrani kubwa kwa baadhi ya watu waliokuwepo maeneo hayo  walionesha juhudi kuuzima moto huo lakini kwa bahati nzuri kikozi cha zima moto kikawa kimeishawasili na kuendelea kupambana na moto huo uliokuwa ukiwaka kwa kasi kubwa mpaka.

Moto ukiteketeza soko hilo.

Kwa upande mwingine wananchi wameonekana wakimwaga machozi na kulitupia lawama kwa Jeshi la Polisi kwa kutowaruhusiwa  kusogea eneo la tukio kuokoa mali zao na kuwafyatulia risasi hewani wakati wa uokoaji.

Moto ukiteketeza soko hilo.

Hii ni mara ya tatu sasa ambapo soko hili liliisha ungua mara mbili mfululizo kabla ya  kuungua tena kwa mara nyingine  usiku wa kuamkia leo.

Hatari! Moto Mkubwa Wateketeza Kabisa Soko la Sido, Mbeya

Leave a Comment