Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hamphrey Polepole (katikati) akiwa amejumuika na waombolezaji.Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers, Eric Shigongo (kushoto) na Mhariri Mtendaji wa kampuni hiyo, Saleh Ally wakiwa msibani hapo.Taswira ilivyoonekana msibani hapo.Mmiliki wa Blog ya Michuzi, Muhidin Issa Michuzi (katikati kutoka kulia ) akiwa na waombolezaji msibani hapo.Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha ITV, Spensa Lameck akitoa heshima za mwisho.Waombolezaji mbalimbali wakitoa heshima za mwisho.Mhariri Mwandamizi wa Gazeti la Uwazi, Elvan Stambuli akiuaga mwili wa Mayage.Mhariri wa Gazeti la Championi Jumatano, Philip Nkini akitoa heshima za mwisho.Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers, Eric James Shigongo akiweka ua la maua katika kaburi la marehemu Mayage.…Shigongo akitoa heshima za mwisho.…Akijiandaa kuweka ua kaburini.Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye akiweka shada la maua kwenye kaburi.Waombolezaji wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu.Padre wa Kanisa Katoliki, John Kaniki akiongoza misa ya kuombea mwili wa marehemu Mayage S. Mayage katika makaburi ya Mbweni jijini Dar es Salaam.Mjane wa marehemu aitwaye, Digna Mayage akiwa ameshikiliwa na waombolezaji akielekea makaburini.Wapiga picha kutoka Ikulu, Muhidin Issa Michuzi na John Chacha wakiweka shada la maua.Jeneza lenye mwili likiingizwa kaburini.Picha ya Mayage enzi za uhai wake.
WANAHABARI nchini wameombwa kuendeleza amani na upendo katika kumuenzi marehemu, Mayage S. Mayage liyefariki dunia juzi jijini Dar es Salaam kama ishara ya kuiga matendo mema aliyoyatenda enzi za uhai wake.
Hayo yamesemwa leo na Padre John kaniki wa Kanisa Katoliki katika ibada fupi ya mazishi ya kumuaga Mayage iliyofanyika nyumbani kwake Mbweni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Akiendesha misa hiyo, Padre Kaniki alisema msiba ni sehemu ya kujifunza kutenda yaliyo mema kwa wale wanaobaki hivyo ni vyema wote kuwa wanyenyekevu kwa Mungu.
Kwa upande wa familia ikisoma risala ilisema kuwa wakati wa uhai wake marehemu alisoma katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi na baada ya kuhitimu alifanya kazi katika maeneo mbalimbali.
Naye Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Saleh Ally akizungumza kwa niaba ya kampuni amaemuelezea marehemu kama mwandishi aliyeacha alama ya ujasiri na uthubutu katika tasnia ya habari kwani ni alitanguliza mbele maslahi ya kazi kuliko vitu vingine na hivyo akasema ni pigo kwa familia na jamii kwa ujumla