×

ALICHOKISEMA HAKIMU KWENYE HUKUMU YA SCORPION

Scorpion akipelekwa mahakamani leo.

Hukumu ya mwalimu wa sanaa ya kujihami ‘martial arts’  Salum Njwete maarufu kama Scorpion, ya kumjeruhi na kumtoboa macho kinyozi Said Mrisho leo ilishindwa kusomwa katika Makahama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar kufuatia hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, Flora Haule, kusema bado hajakamilisha kuiandaa.

Majeruhi Said Mrisho aliyetobolewa macho (katikati) akiongozwa na ndugu zake kuondoka makamani hapo baada ya kesi hiyo kuahirishwa.

Hakimu huyo ameiharisha kesi hiyo mpaka Januari 22 mwaka huu ambapo amesema atatoa hukumu hiyo.  Kufuatia hali hiyo, Scorpion amerudishwa rumande mpaka tarehe hiyo.

Said Mrisho akiingia kwenye Bajaj kurejea nyumbani.

 

PICHA: RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY / GPL

 

VIDEO: Kilichotokea Mahakamani Kwenye Hukumu ya Scorpion Leo