×

Azam FC Yapewa Kandarasi Mpya na NMB

Mkurungezi wa NMB, Imeko Bussemaker (kushoto), akikabidhi mkataba huo kwa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Azam FC, Abdul Mohamed ndani ya makao makuu ya ofisi hizo Posta jijini Dar es Salaam, mapema leo.

 

KLABU ya Soka ya Azam yaneema tena na mkataba mpya wa NMB baada ya kuonekana kuutendea haki mkataba wao wa awali wa benki hiyo hivyo imewaongezea mwingine wa mwaka mmoja ambao utawasaidia kupambana kuchukua Ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.

 

 

Wakurugezi na baadhi ya wafanyakazi wa NMB,wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiana mkataba huo.

 

Akizungumza wakati wa kusainishana mkataba huo Mkurungezi wa NMB,Imeko Bussemaker, alisema kwamba wameamu kuingia mkataba mpya na Azam baada ya kuridhishwa na ule wa awali, hivyo kwakuwa wao wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika masuala ya michezo,wanaamini Azam itaongeza wigo mkubwa katika kuzalisha wachezaji wachanga hapa nchini ambao wataiinua hata timu ya taifa wanayoidhamini pia.

 

Mkurungezi Mkuu wa NMB,Imeko Bussemaker (kushoto), akisaini mkata huo sambamba na Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Azam FC, Abdul Mohamed.

 

Naye Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdul Mohamed, yeye amewashukuru NMB kwa udhamini huo “Niwashukuru sana kwa hili lakini huku napenda niwaahidi kua siku chache zijazo nitarudi hapa tena kuwakabidhi Kombe la Ligi Kuu Bara, kwani tunaamini hadi  mwisho wa msimu mambo yatanyooka maana farsafa yetu kwa sasa tunaendelea kupambana kimyakimya kama tunamfukuza mwizi,” alisema Abdul.

 

Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Azam FC, Abdul Mohamed (kulia), akimkabidhi Mkurungezi Mkuu wa NMB,Imeko Bussemaker moja ya jezi zinazotumiwa na klabu hiyo msimu huu.

 

Baadhi ya wanahabari wakitekeleza wajibu wao wakati wa makabidhiano ya mkataba huo.

 

Nahodha wa timu ya Azam FC, Himidi Mao (kushoto), akimkabidhi kombe lao waliloshinda kwenye michuano ya mapinduzi Cup Mkurungezi Mkuu wa NMB,Imeko Bussemaker baada ya shughuli za kusainishana mkata mpya kumalizika.

 

Habari/Picha: Musa Mateja/GPL