
NDUGU, jamaa, marafiki na Watanzania wengine wamejitokeza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kuuchukua mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini ambaye ataagwa leo katika viwanja vya chuo hicho.

Taswira halisi inaonyesha ndugu wakifanya maandalizi ya kuchukua mwili wa Akwilina na kabla ya kuupeleka NIT ambako utaagwa na baadaye nyumbani kwao Mbezi kisha kusafirishwa kwenda Rombo kuzikwa.

Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.




PICHA NA DENIS MTIMA | GPL
LIVE: MWILI WA ‘AKWILINA’ UKICHUKULIWA MUHIMBILI (VIDEO)