×

Mwili wa Akwilina Wawasili Kwao Rombo – Video

Wanafunzi ambao alikuwa akisoma nao marehemu Chuo cha NIT wakiwa msibani hapo. Wa kwanza kushoto ni mshauri wa wanafunzi, Paulina  Tarazo, Agripina  Joseph, Beatrice  Charles na Komba Anthony wakiwawakilisha wenzao. 

MWILI wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), Akwilina Akwilini umewasili nyumbani kwao Rombo-Mashati mkoani Kilimanjaro leo Alhamisi, Feb. 23, 2018 majira ya saa 1: 45 asubuhi kwa ajili ya mazishi.

Hali ilivyo nyumbani kwa marehemu.

 

Akiongoza msafara wa waombolezaji waliopeleka mwili huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo na Mkuu wa Chuo cha NIT, Prof. Zakaria Mganilwa wamekabidhi mwili huo kwa familia.

Mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani hapo.

Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu, shughuli ya kuaga mwili wa marehemu itaanza saa 5:00 asubuhi ambapo mwili utapelekwa kanisani kwa ajili ya ibada ya kuagwa na mazishi yatafuata.

Rafiki wa marehemu wakiwa msibani hapo.

 

Aidha, kwa sasa wanaosubiriwa ili kuendelea na shughuli hiyo ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Ndalichako, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, makatibu wakuu na manaibu makatibu wakuu, Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini na viongozi wengine.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza na waombolezaji wengine.

 

Akwilina aliagwa jana Alhamisi katika viwanja vya NIT vilivyopo Mabibo, Dar es Salaam na kusafirishwa kwenda kijini kwao.

Mwili ukiwasili.

 

Mwanafunzi huyo alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema).
Akwilapo akikabidhi mwili.

 

Waombolezaji wakikusanyika nyumbani kwao marehemu.

 

Waombolezaji wakiwa wenye huzuni msibani hapo.

 

Mwili ukiwasili nyumbani.

 

Kaburi ambamo atazikwa marehemu.

 

PICHA NA VICTOR MOSHI | GLOBAL TV, ARUSHA

Mwili wa Akwilina Wawasili Kwao Rombo